KITAA SHOP |Bofya Picha Kutembelea Kitaa Shop

Saturday, August 31, 2013

Kipaji kinachoota kwa kasi toka Makambako-Njombe.

Kipaji Kinachoota kwa kasi toka Makambako - Njombe. Artist anaeweza na anafanya Music wa Hip Hop. Katoka na Track iitwayo Labda Kesho ft J- Melody toka 05 Records. Video ya track hio inataraji dondoka soon mtaani. Tembelea link hapo chini kuisikiliza, share ama download track hio. Support yako ndo kila kitu mdau.

http://www.hulkshare.com/5krps75f9vuo

Mjue Mtangazaji Na Dj Waloinua zaidi Music Nyanda za Juu kusini 2006-2013 mwanzoni.

 Moja kati ya watangazaji walofanikiwa leta mabadiliko makubwa ya Music Nyanda za Juu kusini, Eddo Bashiri akiwa kwenye kipindi chake cha One six show wakati huo bwana.
 Dj Mkali, na alie leta Mabadiliko Makubwa nyanda za Juu Kusini Kwa sasa yupo Dar Capital Radio akipiga kazi huko. Miss u Muba coz unatukumbusha Mengi. Alikua rafiki Mkubwa wa Eddo Nje ya kufanya kazi wote.
 Alikua kipenzi cha wengi wakati akitangaza, Na hata sasa bado anauliziwa saaaana Mtaani na wasikilizaji kibao. Kudhihirisha haya, Makonda madereva, wa daladala, vijana mitaani wamekua wakitumia moja ya sauti zake akiwa kwenye kipindi kama Miito ya simu kwenye simu zao. Hili nimeweza lishuhunia mwenyewe. Moja ya sauti hizo utaipata hapa hapa kwenye ukurasa huu.
Hapa akiwa nje ya Ofice yake Radio Ebony fm wakati anatangaza hapo.

Bado tunakupenda, na tunakukumbuka sana. Hope ipo siku watu mtajua kwanini niliamua makala ya Mtangazaji huyu, na Dj Muba ambae walikua kama Mapacha Ama kam Tom And Jerry kwa wale wapenda katuni. We Miss u Bro Kitaaaa.


http://www.hulkshare.com/w4411up48s1s

Sehemu ya pili ya Mafanikio ya Msanii Mgc Mtata.

 The Sky English Medium, Moja ya madarasa ya Shule hio kwa sasa ambayo yanaendelea tumika na yako Chini ya Artist Mgc Mtata Mzee wa Kauli Ifunda Iringa.
 Baadhi ya wanafunzi wanaosoma Hapo Masomo ya QT na Kurudia Mitihani ya kidato cha nne.

 Darasa kwa ndani jinsi lilivyo,

Wote Mnakaribishwa. Haya ndio yalikua baadhi ya Mafanikio na Miradi ya Msanii tajiri kuliko wote nyanda za juu kusini Mgc-Mtata, ambae anamtaji wa takribani 120 Million anazo miliki kwenye mali zake.